Serikali
 imesema Shirika la Umeme nchini (Tanesco), liendelee kukata umeme kwa 
wateja sugu wanaodaiwa malimbikizo ya Ankara zao za hata kama ni taasisi
 nyeti za serikali.
Waziri
 wa Nishati, Dk. Medard Kalemani ameyasema hayo kutokana na maombi 
maalumu yaliyotolewa na Mkuu wa Gereza la Handeni Miraj Katumbili na 
Meneja wa Mradi wa Maji wa HTM, Yohana Mgaza, waliotaka umeme usikatwe 
katika ofisi zao na wizara wakati zikitafuta ufumbuzi wa kulipa 
malimbikizo ya madeni yao.
Mrakibu
 Mwandamizi wa jeshi la Magereza SSP Katumbili, alisema mara nyingi 
umeme unapokatwa katika gereza hilo wanakuwa na wakati mgumu kutokana na
 aina ya watu wanaofungwa kwa makosa mbalimbali, hivyo wangeomba 
wasikatiwe.
Kwa
 upande wake Mgaza, alisema mradi wao wa maji wa HTM licha ya kukabiliwa
 na changamoto mbalimbali, wanakiri kwamba Tanesco wanawadai zaidi ya Sh
 milioni 900 ambazo Wizara ya Maji imeanza kulipa lakini wamekuwa 
wakikatiwa umeme mara kwa mara.
“Mheshimiwa
 Waziri sisi ni wateja wakubwa wa Tanesco, tunawahudumia wananchi kwa 
maana tunatoa huduma, ni kweli tunadaiwa zaidi ya Sh milioni 900, wizara
 yetu imejitahidi kulipa kiasi cha Sh milioni 500 lakini bado tunakatiwa
 umeme wananchi hawapati maji,” amesema Mgaza.
Naye
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe, akichangia suala hilo alisema
 anasikitishwa na Ofisi ya Tanesco Mkoa wa Tanga, namna wanavyoshindwa 
kukaa pamoja kutafuta suluhisho la kudumu la kutatua tatizo hilo ambalo 
kimsingi kwa vile wizara imeanza kulipa linazungumzika.
“Wizara
 ilishaanza kuonesha jitihada za kumaliza deni lakini wanakata umeme na 
wananchi wanakosa huduma hii muhimu, nimeongea na ofisi ya mkoa kumaliza
 tatizo hili, nimelalamika kwenye kikao ch RCC nikitaka wakutane 
walimalize, lakini hadi leo Tanesco hawataki kukaa pamoja,” amesema Mkuu
 huyo wa Wilaya.
Akifafanua
 hilo Dk. Kalemani aliwapongeza kwa kuonesha jitihada za kulipa lakini 
akasisitiza madeni hayo lazima yalipwe kwa kuwa Shirika hilo na lenyewe 
limekuwa na madeni mbalimbali ya zaidi ya Sh bilioni 700 huku lenyewe 
likidai kwa wateja wake kiasi cha Sh bilioni 200.
“Ni
 kweli tunajua wananchi wanaumia lakini mnapolipa Ankara hizi inasaidia 
kuliwezesha shirika kuwasaidia wananchi kwa kuwasambazia nishati ya 
umeme,” amesema Waziri na kumwagiza Meneja wa Tanesco Mkoa wa Tanga, 
Julius Sabu, kuwafuata viongozi wa HTM kumaliza suala lao mapema 
iwezekanavyo.






No comments:
Post a Comment