Serikali
 imezitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatoa vibali vya ujenzi
 wa nyumba ndani ya siku tatu na kazi hiyo isimamiwe na Maofisa Mipango 
Miji.
Aidha,
 imesisitiza kuwa zoezi la urasimishaji katika maeneo yaliyojengwa 
nyumba kiholela lazima yarasimishwe na zoezi hilo halitakiwi kubomoa 
nyumba ya mtu yoyote.
Kauli
 hiyo imetolewa jana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 
William Lukuvi wakati akifungua mkutano wa tano wa Bodi ya Wataalamu wa 
Usajili Mipango Miji unaoendeleo katika jiji la Dodoma.
Lukuvi
 alisema vibali vya ujenzi wa nyumba katika maeneo mbalimbali lazima 
vitolewe aidha katika eneo lililopangwa ama lisilo pangwa na cha msingi 
serikali inachotaka ni kuwa na majengo yaliyo katika mpangilio mzuri na 
kuongeza kuwa ucheleweshwaji wowote utoaji kibali lazima mhusika 
afahamishwe sababu za kucheleweshewa kupatiwa kibali.
Kwa
 mujibu wa Lukuvi lengo la Maofisa Mipango Miji kupewa mamlaka ya kutoa 
vibali vya ujenzi badala ya wakuu wa idara wa halmashauri husika 
linatokana na baadhi yake kuongozwa na watu wasiokuwa na taaluma za 
mipango miji jambo linaloweza kuvuruga upangaji miji bora kwenye maeneo.
Pia
 ametaka nakala za vibali vya ujenzi vitakavyotolewa na kuhakikisha 
nakala hizo za vibali zinaenda pia katika ofisi za maafisa watendaji wa 
mitaa kwa kuwa watendaji hao wanapaswa kufahamu ujenzi unaoendelea 
katika maeneo yao.
Lukuvi
 ameitaka Bodi ya Usajili Mipango Miji kuandaa muongozo utakaosaidia 
watendaji wa mitaa kuwa na ufahamu katika kusimamia mipango ya 
uendelezaji miji jambo litakalosaidia pia kuepuka   ujenzi holela katika
 baadhi ya maeneo.
Akigeukia
 suala la urasimishaji maeneo yasiyopimwa, Lukuvi alisema pamoja na 
zoezi hilo kufanyika nchi nzima lakini hakuna nyumba itakayovunjwa 
katika zoezi hilo na kutaka makampuni yote yatakayotaka kufanya kazi ya 
urasimishaji kutuma maombi yao kupitia ofisi za wilaya na kuacha kuenda 
moja kwa moja kufanya kazi hiyo kupitia kamati maalum za maeneo husika 
na kusisitiza kuwa zoezi hilo lazima liratibiwe na Maofisa Mipango Miji.
Katika
 hatua nyingine, Lukuvi amepiga marufuku upimaji mashamba katika maeneo 
mbalimbali bila ya kupangwa na kubainisha kuwa serikali haitakubali 
kadhia hiyo iendelee kushamiri kwani suala hilo linafanya miji kukosa 
maeneo ya wazi, mashule, masoko na hospitali.
Salfonce
 Kesi Mtafiti na mwalimu katika Chuo cha Ardhi alisema, kwa sasa mambo 
mengi ya upangaji miji katika maeneo mbalimbali nchini hayaendi vizuri 
kutokana na mipango kufanywa na watu wasio na taaluma ya mipango miji.
Alisema,
 ni lazima suala la mipango miji katika maeneo lianze ndipo mipango 
mingine ya maendeleo iendelee kama vile huduma za maji, barabara pamoja 
na huduma nyingine za jamii.
Mwenyekiti
 wa Bodi ya Usajili Mipango Miji Profesa Wilbert Kombe alisema bodi yake
 imeanza kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha taaluma ya Mipango Miji 
inakuwa na wataalamu wanaozingatia sheria na kuchangia kuwepo miji bora 
na iliyopangika na kubainisha kuwa mahali popote sura ya miji ndiyo 
inayotoa taswira ya maisha ya eneo husika.






No comments:
Post a Comment