Abiria wawili Raia wa Sudan Kusini na Syria jana wamekamatwa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) wakisafirisha fedha taslim dola 70,000 za Kimarekani sawa na shilingi milioni 156 za Kitanzania na paundi 3410 za Sudan bila kufuata taratibu.
Akizungumza
 na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la 
abiria la JNIA, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi, Barnabas 
Mwakalukwa alimtaja Raia wa Sudan Kusini Bi. Nada Zaelnoon Ahamed (38) 
mwenye hati ya kusafiria namba P01563534 amekamatwa saa 10:00 jioni 
akiwa eneo la ukaguzi wakati akiingia ndani tayari kusafiri kwa ndege ya
 Shirika la Ndege la Kenya (KQ 485) akielekea Nairobi.
Hatahivyo,
 Afande Mwakalukwa amesema abiria huyo amekamatwa na dola 60,000 za 
Kimarekani na paundi za Sudan 3410, ambazo zote kwa pamoja alishindwa 
kutoa taarifa ya fedha alizokutwa nazo kwa mujibu wa sheria ya 
utakatishaji fedha ya mwaka 2006 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2012.
Pia
 alimtaja Bw. Mohamed Belal (31), Raia wa Syria mwenye hati ya kusafiria
 namba 003-16L096876 aliyekuwa akisafiri kwa ndege ya Shirika la ndege 
la Ethiopia (ET 864) kuelekea Syria kupitia Addis Ababa amekamatwa na 
dola za kimarekani 10,000 sawa na Tsh. milioni 20 za Kitanzania, ambazo 
naye alishindwa kuzitolea taarifa.
“Watuhumiwa
 wote wawili wamezuiwa na hawawezi kuendelea na safari zao kwa ajili ya 
uchunguzi zaidi na hatua za kisheria zilizopo,” amesema Afande 
Mwakalukwa.
Naye
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. 
Richard Mayongela amewapongeza maafisa usalama wa JNIA kwa kufanya kazi 
kwa weledi na uadilifu pamoja na kushirikiana na vyombo vingine vya 
ulinzi na usalama katika kuhakikisha wasafiri, wadau na maeneo yote ya 
viwanja vya ndege yanabaki salama na vitendo vya kiuhalifu havina nafasi
 katika viwanja hivyo.
Bw.
 Mayongela amesema pamoja na watumishi hao kufanya kazi katika wakati 
mgumu kutokana na baadhi ya abiria kuwa watata kila wanapotaka 
kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na kanuni.






No comments:
Post a Comment