JAMII WILAYANI KAHAMA YATAKIWA KUACHANA NA IMANI POTOFU YA KUWAKATA WATOTO NDIMI ZAO


Na Salvatory Ntandu
KAHAMA

Jamii wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA imetakiwa kuondokana na imani potofu za kuwata watoto wachanga ndimi ili kuzuia kupata tatizo la kuzungumza(Ububu) jambo ambalo linaweza kusababisha vifo na kigugumizi wakati wa kuzungumza.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa kitengo cha Meno katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa KAHAMA DK ATHUMANI HUSEIN JUMA wakati akizungumza na KAHAMA FM kuhusiana na suala hilo.

Amesema ofisi yake imebaini kuwepo kwa Mama mmoja anayejifanya ni mtaalamu wa kukata watoto wachanga ndimi pindi wanapozaliwa jambo ambalo linasababisha madhara kwa watoto.

Amefafanua kuwa Tatizo la kuzungumza kwa mtoto (Ububu) linatokana mtu kuwa na tatizo kwenye ubongo hivyo wapaswa kutowapeleka watoto wao.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuwepo kwa watoto wachanga ambao wamebainika kukatwa ndimi zao kwa kile kinachodawa kuwa ni kuzuia tatizo la Ububu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive