WANAWAKE ZAIDI YA ASILIMIA 70 WANAOTIBIWA HOSPITALI YA WILAYA KAHAMA HUSUMBULIWA NA MAGONJWA YA KINYWA


Na Sebastian Mnakaya
KAHAMA.

Zaidi ya asilimia 70 ya wanawake wanaotibiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, wanasumbuliwa na magongwa ya kinywa kutokana na ulaji wa vyakula vitamu mara kwa mara hali inayosababisha meno yao yatoboke.

Hayo yameelezwa na mganga wa meno kutoka katika Hospital ya halmashauri ya mji wa Kahama, DR ATHUMANI HUSSENI JUMA katika mahojiano na kahama FM kuhusiana na maadhimisho ya siku ya kinywa na meno duniani leo.

Kwa mujibu wa Dk. JUMA, watoto wa umri wa miaka 2 mpaka watu wazima walio na umri wa miaka 45 wako kwenye hatari zaidi ya kupata magonjwa ya kinywa na meno wasipozingatia afya ya kinywa.

Dk JUMA ametoawito kwa Wananchi kuwa na utaratibu wa kuangalia afya zao za kinywa na meno mara kwa mara na kupata matibabu mapema kuepuka kupata kansa ya kinywa.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive