WANANCHI ISAGEHE WAIOMBA HALMASHAURI KUMALIZIA BOMA LA OFISI YA SERIKALI YA KIJIJI


Na Ndalike Sonda
KAHAMA

Wananchi wa Kijiji cha MPERA kata ya ISAGEHE Halmashauri ya Mji wa KAHAMA wameiomba halmashauri hiyo kumalizia boma la ofisi ya serikali ya kijiji hicho baada ya kutelekezwa kwa zaidi ya miaka 13.

Wakizungumza jana na KAHAMA FM kwa niaba ya wananchi wengine, MANYANDA NDUBA na ALFERD HUNGWI wamesema wananchi walihamasishwa kuchangia ujenzi huo tangu mwaka 2005 ambapo walikamilisha boma hilo.

Mwenyekiti wa serikali ya Kijiji hicho, ALON MAKINGA amesema taarifa za ukamilishaji wa bomba hilo zipo kwenye ofisi ya halmashauri ya Mji wa Kahama na kwamba wananchi wamesaidia pia upatikanaji wa mbao za kenchi na bando mbili za mabati.

Afisa Uchumi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama ANGERIA CLAVERY amesema jengo hilo halijakamilika kutokana kipaumbele cha ujenzi wa vyumba vya madarasa na katika mwaka wa fedha 2017/18 wametenga kiasi cha shilingi milioni 15 kwaajili ya ukamilishaji wa jingo hilo.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive