WANANCHI WA PUGU BUKONDAMOYO MJINI KAHAMA WAMEKUBALI KUCHANGIA FEDHA KWA AJILI YA MAENDELEO YA KIJAMII.



Na Ndalike Sonda
KAHAMA.


Wananchi wa Kitongoji cha Pugu mtaa wa Bukondamoyo mjini Kahama wamekubaliana kuchangia fedha na nguvu kazi ili kufanikisha uwekaji wa changarawe na mawe kwenye daraja lililopo katika kitongoji hicho, ili kuwezesha barabara hiyo kuanza kutumika.

Wakizungumza leo kwenye kipindi cha Raha ya leo kinachorushwa na Kahama FM baadhi ya wananchi wamesema kutokana na kero ya barabara inayowakabili kwa muda mrefu, serikali ya mataa iliitisha mkutano na wananchi, na kupitisha maazimio hayo.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Bukondamoyo NASHONI YOHANA amesema daraja hilo limejengwa tangu mwaka jana na hakuna mwendelezo wowote na kwamba wanakusudia kukamilisha baada ya wiki moja ili barabara hiyo ianze kutumika.

Diwani wa kata ya Mhungula IGNAS SHABAN amewapongeza wananchi hao, na kuahidi kushirikiana nao katika shughuli mbalimbali za maendeleo, ikiwamo ukamilishaji huo wa daraja katika barabara ya kitongoji cha Pugu.

Mkuu wa kitengo cha Uhandisi kutoka wakala wa barabara za mjini na vijijini (TARURA) halmashauri ya mji wa Kahama Mhandisi, YUSUPH SHABAN amesema wananchi wanaruhusiwa kufanya marekebisho hayo lakini wawashirikishe wataalam wanaohusika kutoka TARURA.

Hata hivyo Mhandisi SHABAN amesema TARURA inaendelea kukabarabati barabara mbalimbali zilizopo mjini Kahama kulingana na bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive