SERIKALI WILAYANI KAHAMA YAWATAKA WANANCHI WAISHIO PEMBEZONI MWA MAENEO YA MACHIMBO YA DHAHABU KURIPOTI MATUKIO YA UVUNJIFU WA AMANI


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Serikali wilayani KAHAMA imewataka wananchi waishio katika maeneo ya machimbo madogo ya madini kutoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi na usalama matukio yote yanayoashiria uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

Akizungumza leo kwenye uzinduzi wa kampeni ya utunzaji wa mazingira na upandaji wa miti katika machimbo madogo ya dhahabu ya Kabela Ilindi, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, FADHILI NKURLU amesema kila mchimbaji wa madini anawajibu wa kulinda usalama.

Amesema kutokana na wingi wa watu machimboni, ulinzi hauna budi kuimarishwa sanjari na utunzaji wa mazingira kwa ili kudumisha amani na kuzuia magonjwa ya mlipuko huku akiupongeza uongozi wa Machimbo hayo kwa utunzaji wa mazingira na usalama.

Akizungumza kwa niaba ya Wachimbaji wenzake, SHADRACK NYAMHOKYA amesema wavamimizi wa machimbo wamekuwa wakileta hofu kwa wachimbaji hao na kuiomba serikali kadhibiti hali hiyo ikiwa ni pamoja na kuboresha barabara ya kutoka Kahama kwenda katika machimbo hayo.

Katika zoezi hilo la utunzaji wa mazingira na upandaji wa miti jumla ya miche 500 imepandwa, huku akiahidi kupeleka miche mingine elfu 10 katika machimbo hayo ya dhahabu ya Kabela Ilindi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive