OFISI YA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MSALALA WILAYANI KAHAMA YAOMBA RADHI KWA KUWASILISHA TAARIFA ISIYO RASMI KWENYE KIKAO



Na Amina Mbwambo
KAHAMA

Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya MSALALA wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA imelazimika kuomba radhi katika kikao cha Kamati ya Ushauri cha wilaya ya KAHAMA (DCC) baada ya kuwasilisha mbele ya kamati hiyo taarifa isiyokidhi matakwa ya kikao hicho.

Akiomba radhi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo SIMON BEREGE, Mwanasheria wa Halmashauri, MASHAKA MABULA amesema upungufu uliojitokeza umesababishwa na taarifa za ghafla za yeye kukaimu nafasi hiyo ya Mkurugenzi Mtendaji.

Akizungumzia hali hiyo, Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kahama, FADHILI NKURLU ameitaka Halmashauri hiyo kuwa makini katika kushughulikia taarifa zake kwani tatizo hilo linaonekana kujirudiarudia.

Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho cha Kamati ya Ushauri cha Wilaya ya Kahama akiwemo Diwani wa Kata ya Nyihogo, SHEDRACK MGWAMI na Diwani wa Kata ya ISAKA, GERALD MWANZIA wameeleza kusikitishwa kwao juu ya taarifa hiyo ya Halmashauri ya Msalala.

Katika kikao hicho cha siku moja, Wajumbe wa Kamati hiyo ya Ushauri ya Wilaya ya Kahama pamoja na mambo mengine wamesisitiza umuhimu wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA), kufanya mazungumzo na halmashauri zenye mitambo ya kutengeneza bara bara ili waweze kutumia mitambo hiyo.

Aidha wajumbe wamesisitiza mapendekezo ya bajeti ya halmashauri husika yapitishwe kwenye kamati ya ushauri ya wilaya kabla ya kujadiliwa na madiwani, na halmashauri ziwasilishe maombi serikali kuu ili kuwahishiwa fedha za ruzuku kwa ajili ya kutekeleza bajeti zao.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive