ACACIA YAKABIDHI VIFAA VYA UJENZI KWA HALMASHAURI ZA KAHAMA MJI NA MSALALA

Na Amina Mbwambo
KAHAMA.

Kampuni ya ACACIA kupitia migodi yake ya dhahabu ya BULYANHULU na BUZWAGI Wilayani KAHAMA imekabidhi vifaa mbalimbali vya ujenzi kwa Halmashauri za KAHAMA Mji na MSALALA Wilayani KAHAMA, vyenye thamani ya shilingi milioni 150.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Meneja Mkuu wa migodi hiyo, BENEDICT BUSUNZU amesema wamefikia hatua hiyo baada ya kuguswa na tatizo la uhaba mkubwa wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri hizo zinazoizunguka migodi.

BUSUNZU amesema leo wamekabidhi mifuko ya saruji 3200 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 80 na kwamba vifaa vingine vya ujenzi vitakabidhiwa kwa Halmashauri husika kwa nyakati tofauti kulingana na hatua za ujenzi wa madarasa ili kuinua kiwango cha elimu.

Akipokea msaada huo, mkuu wa wilaya ya KAHAMA, FADHILI NKURLU amesema Halmashauri hizo mbili kwa pamoja zina uhitaji wa vyumba vya madarasa zaidi ya 1500 hivyo msaada huo utasaidia kupunguza tatizo la uhaba huo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kahama Mji ANDERSON MSUMBA na Kaimu mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Msalala, MARY NZUKI wameishukuru kampuni ya Acacia kwa msaada huo.

Kampuni ya Acacia kupitia migodi ya dhahabu ya Buzwagi na Bulyanhulu imedhamiria kujenga vyumba vya madarasa zaidi ya 1575 katika awamu hii, kwenye shule za msingi 84 na za sekondari 30 katika Halmashauri hizo za Msalala na Kahama Mji.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive