KIASI CHA SHILINGI MILIONI 54 KIMEGAWIWA SHULE ZA MSINGI HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA


Na Ndalike  Sonda
KAHAMA.

Jumla ya shilingi milioni 54 zimegawiwa katika shule za msingi 36 kati ya 72 za Halmashauri ya Mji wa KAHAMA kwa lengo la kuziwezesha kuendesha miradi mbalimbali ya kujitegemea shuleni.

Akizungumza na KAHAMA FM, Kaimu Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji wa KAHAMA, PEREPETUA MAYIGE, amesema fedha hizo zimetolewa na Mpango wa kuboresha elimu Tanzania (EQUEP Tanzania) ambapo kila shule imepata shilingi milioni 1.5.

MAYIGE amesema lengo la mpango huo ni kuhakikisha kila shule ina kuwa na miradi ya kujitegenea ambayo itasaidia upatikanaji wa chakula cha wanafunzi shuleni na hivyo kuongeza kiwango cha ufaulu katika halmashauri hiyo.

MAYIGE amesema ukosefu wa chakula cha wanafunzi shuleni ni changamoto ambayo inasababisha baadhi ya wanafunzi kushindwa kumudu masomo na kwamba jamii inapaswa kushirikiana na shule ili kuatatua changamoto hiyo.

Halmashauri ya mji wa Kahama inajumla ya shule za msingi 72 za serikali zenye wanafunzi zaidi ya 68 elfu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive