AHUKUMIWA KWENDA JELA AU KULIPA FAINI KWA KOSA LA KUINGIA IFADHINI BILA KIBALI


Na Lilian Katabbaro
KAHAMA

Mkazi wa Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, JACOB MASUMBUKO (44) jana amehukumiwa kwenda jela mwaka mmoja au kulipa faini ya shilingi 350,000/= kwa kosa la kuingia ndani ya Pori la Akiba la Moyowosi-Kigosi bila kibali.

Akitoa Hukumu hiyo, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Kahama IMANI BATENZI amesema ametoa hukumu hiyo baada ya mshitakiwa MASUMBUKO kukiri kutenda kosa hilo Mahakamani hapo.

Awali mwendesha mashitaka wa Idara ya Wanyamapori CATHERINE ALOYCE amesema MASUMBUKO alikamatwa March 16 mwaka huu huko Bulumbaga ndani ya Pori hilo la Akiba la Moyowosi-Kigosi akiwa hana kibali kinachomruhusu kuwa katika eneo hilo.

ALOYCE amesema katika shauri hilo la jinai namba 120/2018, MASUMBUKO ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 15 cha sheria ya wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009.

MASUMBUKO ameshindwa kulipa faini na ameanza leo kutumikia kifungo chake jela.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive