SERIKALI WILAYANI KAHAMA KUENDESHA MSAKO WA WAFANYABIASHARA WA MBAO, ALMINIUM NA WACHOMELEAJI.





Na Salvatory Ntandu
KAHAMA


Serikali wilayani KAHAMA imesema itaendesha msako wa wafanyabiashara wa mbao, alminium na wachomeleaji vyuma ambao wamekaidi kuhamia katika eneo jipya walilotengewa la Dodoma baada ya kukamilisha uwekaji wa miundo mbinu muhimu ukiwemo umeme katika eneo hilo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya KAHAMA, FADHILI NKURLU wakati akizungumza na Waandishi wa habari Mjini humo ambapo amesema wapo baadhi ya wafanyabiashara ambao hawataki kuhamia katika eneo hilo.


NKURLU amesema ofisi yake imepokea taarifa za baadhi ya wamiliki wa nyumba mjini Kahama kuwapangisha kwa siri watu wanaochomelea vyuma katika Nyumba zao licha ya kutambua madhara yatokanayo na moto.

Kwa upande wao baadhi ya mafundi wanaochomelea katika eneo la Lumambo, RASHID OMAR na ISSA JUMA wamesema wao hawapingani na agizo la serikali ila wanachoomba ni kuboreshewa mazingira ya kazi katika eneo hilo la Dodoma.

Mwaka jana Halmashauri ya mji wa Kahama iligawa viwanja zaidi ya 400 katika eneo la Dodoma kwa wafanyabiashara wa mbao, aluminum na wachomeleaji vyuma baada ya eneo lao la awali la Majengo kuteketezwa kwa moto.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive