MICHE YA MITI INAYOOTESHWA KWA AJILI YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA YAARIBIWA NYASUBI SHULE YA MSINGI


Na Ndalike Sonda
KAHAMA

Miche ya miti inayooteshwa kwaajili ya utunzaji wa mazingira katika shule ya msingi Nyasubi Mjini KAHAMA imeelezwa kuharibiwa na mifugo kutokana na ukosefu wa uzio katika shule hiyo.

Hayo yamesemwa na Mwalimu wa Mazingira wa shule hiyo RACHEL IRUGA wakati akizungumza kuhusu utanzaji wa miti shuleni hapo, kwenye kipindi cha Raha ya leo kinachorushwa na KAHAMA FM.

Kutokana na changamoto hiyo, Mwalimu IRUGA ameiomba serikali kusaidia kujenga uzio katika eneo la shule hiyo ili kudhibiti uharibifu wa mazingira unaotokana na baadhi ya wananchi kuchungia mifungi yao katika eneo la shule pamoja na wapita njia.

Akizungumzia tatizo hilo, Mkazi wa Mtaa wa Nyakato ilipo shule hiyo, RASHID ATHUMAN ameiomba serikali itoe elimu shirikishi kwa wananchi ili wasaidie kulinda na kutunza maeneo ya shule.

Afisa Elimu shule za Msingi Halmashauri ya Mji wa Kahama, ALUKO LUKOLELA, amesema shule ni mali za wananachi hivyo ni jukumu lao kushirikiana kutunza mazingira na kwamba kutokana na kipaumbele cha vyumba vya madarasa hawawezi kujenga uzio huo kwa sasa.

Kukosekana kwa uzio katika shule nyingi za Serikali kumesababisha uharibifu wa mazingira, wizi na uvamizi wa maeneo ya shule.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive