BEI YA NYANYA YAPANDA MASOKO YA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA


Na Sebastian Mnakaya
KAHAMA.

Upatikanaji wa nyanya umekuwa mgumu katika Halmashauri ya Mji wa KAHAMA na kusababisha kupanda kwa bei ya biadhaa hiyo kutoka shilling Elfu kumi na tano hadi elfu ishirini na mbili kwa ndoo kubwa.

Kwa mujibu wa ufuatiliaji uliofanywa na KAHAMA FM katika masoko mbalimbali ya Halmashauri ya Mji wa KAHAMA, hali inawafanya Wafanyabiashara wa rejareja kupandisha bei kwa watumiaji wa bidhaa hiyo.

Wakizungumza na KAHAMA FM kwa nyakati tofauti wafanyabiashara wa soko kuu mjini Kahama wamesema kutokana na uhaba wa nyanya katika mikoa mingine nchini, wafanyabiashara wa nyanya wa mikoa hiyo wanakuja kununua bidhaa hiyo kwa wakulima wa Kahama.

Kwa upande wao wanunuzi na watumiaji wa nyanya waliozungumza na Kahama FM wamewaomba wafanyabiashara kupunguza kidogo bei hiyo ya nyanya kutokana na hali ilivyo ngumu.

Kutokana na upungufu huo wa nyanya, sado moja iliyokuwa ikiuzwa shilingi elfu tatu sasa inauzwa shilingi elfu nane wakati ndoo kubwa ambayo ilikuwa ikiuzwa shilingi elfu kumi na mbili sasa inauzwa shilingi elfu ishirini na mbili.

Aidha ufuatiliaji uliofanywa na Kahama FM umebaini kuwa bei ya sado moja la nyanya katika masoko mbalimbali nchini ni kati ya shilingi elfu saba hadi elfu kumi ikiwa ongezeko la takribani shilingi elfu tatu huku kasha kubwa la nyanya likiuzwa shilling elfu sabini hadi laki moja.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive