AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUBAKA MWANAFUNZI.



Mkazi wa kijiji cha Ntobo Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA, BARAKA CHALESI (19) jana amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi na kumsababishia ujauzito kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo KENETH MUTEMBEI, mwendesha mashitaka wa Polisi EVODIA BAIMO amesema, CHALESI kwa nyakati tofauti mwezi Novemba 2017 huko kijiji cha Ntobo bila uhalali alimbaka mwanafunzi huyo na kumsababishia ujauzito.

BAIMO amefafanua kuwa CHALESI ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 130 na 131 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002, na kifungu cha Sheria ya Elimu namba 60 A sura ya 353 kama ilivyofanyiwa marekebisho na sheria namba 2 ya mwaka 2016.

Katika shauri hilo la jinai namba 107/2018 CHALESI amekana kutenda kosa hilo na upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na mshitakiwa amerudishwa rumande kwa kukosa dhamana hadi shauri hilo litakakapotajwa tena March 23 mwaka huu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive