WATANO WAHUKUMIWA KWENDA JELA AU KULIPA FAINI KWA KOSA LA KUWEPO NCHINI KINYUME CHA SHERIA



Na Paulina Juma
KAHAMA.

Raia watatu wa nchini RWANDA wamehukumiwa kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya shilingi laki tano kila mmoja kwa kosa la kuingia na kuwepo nchini kinyume cha sheria.

Akitoa Hukumu hiyo Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA, KENNETH MTEMBEI amesema ametoa hukumu hiyo baada ya watuhumiwa kukiri kutenda kosa hilo, hivyo watatumikia adhabu hiyo na baada ya hapo watarudishwa kwao Rwanda.

Waliohukumiwa ni pamoja na NIYONZIMA CLAUDE (25), NIYONZIMA TIERI (25) na ALEX CHOYITUNGE (24).

Awali muendesha mashitaka wa Idara ya Uhamiaji SALUM RASHID amesema wote kwa pamoja walikamatwa March 15, mwaka huu huko WENDELE wilayani Kahama wakiwa ndani ya basi la SELECT EXPRESS wakiwa wameingia nichini Tanzania bila vibali vyovyote vinavyowaruhusu.

Katika shauri hilo namba 119 la mwaka huu SALUM amesema wametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 45 cha sheria ya uhamiaji namba 7 ya mwaka 1995 marejeo ya mwaka 2016.

Wote kwa pamoja wameshindwa kulipa faini na wameanza kutumikia kifungo cha miezi sita jela wakimaliza watarejeshwa nchini kwao RWANDA.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive