MADEREVA BAJAJI MTAA WA MHONGOLO WAFUNGA BARABARA KWA MASAA MAWILI



Na Ndalike Sonda
KAHAMA

Ubovu wa barabara ya muda inayotumika kusafirisha abiria kutoka Mjini KAHAMA kwenda Mtaa wa MHONGOLO umesababisha baadhi ya waendesha pikipiki za magurudumu matatu (Bajaji) kufunga barabara hiyo kwa zaidi ya saa mbili, kushinikiza serikali iifanyie ukabarabati.

Baadhi ya waendesha Bajaj wamesema wamelazimika kufunga barabara ili kufikisha kilio chao kwa serikali kwani wamekuwa wakipata usumbufu kutokana na ujenzi wa barabara hiyo ya Mhongolo.

Jeshi la Polisi wilayani Kahama kupitia mkuu wa kitengo cha Usalama barabarani, DESDERY KAIGWA limewaelekeza Madereva hao wa Bajaj kufuata taratibu kwa kupeleka malalamiko yao kwa viongozi wanaohusika kuliko kufunga barabara kwani kufanya hivyo ni kuvunja sjeria.

Kwa upande wake, Meneja wa Wakala wa barabara TANROADS mkoa wa Shinyanga, MIBARA NDIRIMBI amesema hali hiyo inatokana na kutokuwepo kwa mipango miji bora hali inayosababisha maji kuharibu miundombinu hiyo na kwamba amemuagiza mkandarasi kuboresha barabara ya muda.

Barabara hiyo ya muda inayotoka Mjini Kahama kwenda Mhongolo inatumika kutokana na kuwepo kwa ujenzi wa barabara yenye kiwango cha Lami kutoka Mjini Kahama hadi Mhongolo.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive