HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA YASEMA HAMASA YA USAFI WA MAZINGIRA IMEPUNGUA



Na Sebastian Mnakaya
KAHAMA

Halmashauri ya Mji wa KAHAMA Mkoani SHINYANGA imekiri kuwa mwaka huu hamasa ya wananchi wa halmashauri hiyo kufanya usafi wa mazingira katika siku zilizopangwa na Serikali imepungua ukilinganisha na mwaka jana.

Akizungumza na KAHAMA FM, Mkuu wa idara ya Usafi na mazingira halmashauri ya Mji wa Kahama, MARTINE MASELE amesema hali hiyo inatokana na mazoea ya wananchi kusubiri usimamizi wa maafisa kutoka serikalini.

Kutoka na hali hiyo, MASELE amesema wamekusudia kuanza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wanaoshindwa kutekeleza agizo hilo ambapo amewaomba wananchi kuendelea kutii agizo hilo bila shuruti.

Kwa mujibu wa MASELE, zaidi ya tani 121 za takataka zinazalishwa kila siku katika kata 12 zenye msongamano mkubwa wa watu katika mji wa Kahama huku ukusanyaji wake ukiwa ni wakuridhisha.

Zoezi la usafi wa mazingira kila jumamosi ya mwisho wa mwezi ni agizo la rais JOHN MAGUFULI alilolitoa Desemba 9 mwaka 2015 huku wilaya ya Kahama ikitekeleza agizo hilo pia Jumamosi ya katikati ya kila mwezi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive