SHIRIKA LA WORLD VISION LATOA MSAADA KWA VIFAA VYA KUPIMA HALI YA LISHE NA UDUMAVU VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA SH. MIL 100.


Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Serikali Mkoani SHINYANGA imepokea vifaa vya kupima hali ya lishe na udumavu vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 100 kutoka shirika lisilo la kiserikali la World Vision.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya ya KAHAMA, FADHILI NKURLU kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa SHINYANGA, katika Hafla iliyofanyika katika Zahanati ya Kilago katika halmashauri ya mji wa Kahama.

NKURLU amelishikuru Shirika la Word Vision kwa kuchangia maendeleo ya sekta ya Afya mkoani Shinyanga kupitia Mradi wake wa uboreshaji lishe na afya ya uzazi kwa mama na mtoto (ENRICH).

Kwa upande wake, Meneja Mradi wa (ENRICH) MWIVANO MALIBWI amesema wamelenga kuboresha hali ya lishe kwa Mama na mtoto kwa kuwajengea uwezo wa kutambua athari za lishe duni.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Dkt. JOHN MFUTAKAMBA amesema tatizo la udumavu bado ni kubwa, hivyo wazazi wanapaswa kuzingatia lishe bora kwa watoto wao..

Mradi wa ENRICH unatekelezwa katika mikoa mitatu hapa nchini ambayo ni Shinyanga, Tabora na Simiyu na utakamilika mwaka 2020.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive