SHIDEFA KUPIMA WATU LAKI MOJA WENYE UGONJWA WA KIFUA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA PAMOJA NA MSALALA.


Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Katika kuadhimisha Siku ya Kifua Kikuu Duniani Machi 24 mwaka huu, Shirika lisilo la kiserikali la SHIDEFA + linatarajia kupima watu laki moja katika Halmashauri za Mji KAHAMA na MSALALA ifikapo Septemba mwaka huu.

Hayo yamebainishwa leo na Mkurugenzi wa Shirika hilo, VENNANCE MZUKA wakati akizungumza na Waandishi wa Habari mjini Kahama kuhusi utekeleza wa zoezi hilo.

Amesema Utafiti uliofanywa na Shirika hilo umebaini kuwepo kwa dalili za awali za watu wenye viashiria vya ugonjwa huo hususani wanaofanya kazi kwenye migodi midogo na kwenye mikusanyiko ya watu.

Mbali na hilo MZUKA ametoa rai kwa wananchi kuacha dhana potofu kuwa mtu anapopata ugonjwa wa kifua kuku ni kuwa amerogwa jambo ambalo silo la kweli na badala yake waende hospitali kupata tiba.

Shirika la SHEDAFA + litaadhimisha siku hiyo katika mji mdogo wa Isaka, Halmashauri ya Msalala kwa kutoa elimu na huduma ya upimaji bure.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive