AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA UBAKAJI



Na Daniel Magwina
KAHAMA.

Mkazi wa Mtaa wa Majengo Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA, MORGAN SWEBE (32) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya kumbaka mwanafunzi wa miaka 16 na kumsababishia ujauzito kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo KENETH MUTEMBEI, mwendesha mashitaka wa Polisi MASAU MASATU amesema SWEBE kwa nyakati tofauti mwezi Agosti na Septemba 2017 katika mtaa wa Majengo Mjini KAHAMA, alimbaka mwanafunzi huyo na kumsababishia ujauzito.

MASATU amefafanua kuwa SWEBE ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 130 na 131 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002, Na kifungu cha sheria ya Elimu namba 60 A sura ya 353 kama ilivofanyiwa marekebisho na sheria namba 2 ya mwaka 2016.

Katika shauri hilo la jinai namba 133/2018 SWEBE amekana kutenda tuhuma ya kwanza ya kubaka na kukiri tuhuma ya pili ya kumpa ujauzito mwanafunzi huyo.

Upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na mshitakiwa amerudishwa rumande kwa kukosa dhamana na shauri hlo kutajwa tena April 6 mwaka huu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive