RAIA WAWILI WA BURUNDI WAFIKISHWA MAHAKAMANI BAADA YA KUINGIA NCHINI KINYUME CHA SHERIA

Raia wawili wa Burundi jana wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma za kuingia nchini bila kuwa na vibali maalum kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo KENETH MUTEMBEI, mwendesha mashitaka wa Jeshi la Polisi SHABANI MATESO amewataja washitakiwa hao kuwa ni FROLENCE NDAHIZEHE (27) na JANETH MTONELE (22) wote wawili wakiwa ni raia wa BURUNDI.

MATESO amefafanua washitakiwa hao walikamatwa March 6 mwaka huu majira ya saa 7 usiku huko mtaa wa Mwime Wilayani KAHAMA wakiwa hawana kibali kinachowaruhusu kuwemo nchini.

Katika shauri hilo la jinai namba 93/2018, washitakiwa wametenda kosa kinyume na kifungu namba 45 cha sheria ya uhamiaji namba 7 ya mwaka 1995 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016.

Washitakiwa wote kwa pamoja wamekiri kutenda kosa hilo na wamerudishwa rumande baada ya kukosa dhamana hadi March 14 mwaka huu shauri lao litakapotajwa tena.

Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive