WADAU WA ELIMU WILAYANI KAHAMA WATAKIWA KUUNGANA KUTOKOMEZA MIMBA ZA UTOTONI.


Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Wadau mbalimbali wa sekta ya elimu Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA wametakiwa kuunganisha nguvu zao katika kupiga vita ndoa na mimba za utotoni kwa wanafunzi sanjari na kuwafichua watu wanaotekeleza vitendo hivyo kwenye jamii.

Kauli hiyo imetolewa Mjini KAHAMA jana na Mratibu wa Mradi wa uboreshaji wa lishe na afya ya uzazi kwa mama na mtoto (ENRICH) MWALLA MACHIBWA kutoka shirika la World Vision kwenye hafla ya kukabidhi msaada wa vifaa vya kutathimini hali ya lishe mkoani Shinyanga.

MACHIBYA amesema World Vision imeanzisha kampeni hiyo yenye lengo la kutomeza tatizo la mimba kwa wanafunzi na ndoa za utotoni kwa kutoa elimu kwa jamii kuhusu madhara yake.

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Kahama FADHILI NKURLU ambaye alikuwa ni Mgeni Rasmi katika Makabidhiano ya vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidii shilingi milioni 100 amesema hatua kali zitachukuliwa kwa watakaobainika kuwapa mimba wanafunzi.

Mkoa wa Shinyanga ni miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa tatizo la ndoa na mimba miongoni mwa Wanafunzi hapa nchini.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive