SHULE YA MSINGI ISAGEHE YAKABILIWA NA UHABA WA MATUNDU YA VYOO.





Na Ndalike Sonda
KAHAMA


Jumla ya wavulana 339 wanaosoma katika Shule ya Msingi Isagehe Halmashauri ya Mji wa KAHAMA wanakabiliwa na ukosefu wa matundu ya choo hali ambayo imesababisha watumie matundu yaliyokuwa yakitumiwa na wanafunzi wasichana wa shule hiyo. 

Hayo yamebainishwa na Mwalimu mkuu wa shule hiyo, NAMSEMBA MRISHA wakati akipokea msaada wa vifaa vya ujenzi kutoka kwa baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma katika shule hiyo.
 
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mwenyekiti wa wanafunzi waliosoma katika shule hiyo, ZABRON FEGA amesema wametoa mifuko ya saruji 30, Nondo 50 na malori 10 ya mawe vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 2.
 
Mwenyekiti wa Kijiji cha Isagehe, ALEXANDER JOHN na mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, MABALA NKANDI wamesema wameahidi kikamilifu matumizi ya vifaa hivyo ili vitumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

Nao baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Isagehe wamepongeza jitihada zilizofanywa na wanafunzi hao wa zamani wa shule ya Msingi Isagehe na kwamba msaada wao umeleta mwamko kwa wazazi katika kuchangia sekta mbalimbali za maendeleo.

Kwa upande wake, Afisa elimu shule za msingi Halmashauri ya Mji wa Kahama, ALUKO LUKOLELA amesema Halmashauri yake itaendelea kushirikiana na wadau wa sekta ya elimu na kwamba wananchi wanapaswa kutambua kuwa serikali inaruhusu michango ya hiari.
 
Shule ya Msingi Isagehe ilianzishwa mwaka 1939 ambapo kwa sasa inawanafunzi 774 huku ukosefu wa matundu ya choo kwa wavulana ukidumu tangu mwaka 2015.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive