HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA YAANZA KUTOA HUDUMA YA UPIMAJI ARDHI SHIRIKISHI KWA WANANCHI.


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Halmashauri ya Mji wa KAHAMA Mkoani SHINYANGA imeanza kutoa huduma ya upimaji wa ardhi shirikishi kwa wananchi, kwa lengo la kuondoa migogoro ya ardhi inayotokana na wananchi kuuza au kununua maeneo yenye migogoro.

Akizungumza baada ya kutatua mgogoro wa ardhi katika Mtaa wa Bukondamoyo, kutokana na mwananchi mmoja kujenga ndani ya hifadhi ya barabara, Afisa mipango wa halmashauri hiyo IRENE MARO amesema kwa sasa wanatoa elimu juu ya taratibu za ununuzi wa ardhi.

Wakizungumzia mgogoro wa ardhi uliopo baina ya mwananchi na serikali ya mtaa wa Bukondamoyo, ODILIA KAJORO na JOHN MAGANGA wameishauri serikali kuwasimamia maafisa ardhi ili wajenge desturi ya kuwashirikisha wananchi kwenye masuala ya mipango miji.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Bukondamoyo, NASHON YOHANA amesema serikali ya mtaa huo, idara ya ardhi na muuzaji wa eneo lililo na mgogoro wanaangalia namna ya kumfidia mwananchi aliyeuziwa na kujenga kwenye eneo la umma.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive