WAFANYABIASHARA WA VYAKULA MJINI KAHAMA WATAKIWA KUHIFADHI VYAKULA HIVYO KATIKA MAZINGIRA SALAMA.


Na Sebastian Mnakaya
KAHAMA.

Wafanyabiashara wa vinywaji na vyakula vya kufungashwa Mjini KAHAMA wametakiwa kuhifadhi bidhaa hizo kwenye mazingira safi na yasiyo na jua ili visiharibike na kuwaletea madhara watumiaji.

Mratibu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) wilayani KAHAMA, KARISTO KWIWEKO ameiambia KAHAMA FM kuwa tayari amewaandikia barua wafanyabishara hao ambao wamekuwa wakiweka bidhaa hizo nje ya maduka yao kinyume na taratibu za TFDA.

Amewataka Wafanyabiashara hao kufuata sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa na mamalaka hiyo ili kuepuka madhara kwa walaji yanayotokana na kutumia bidhaa ambazo hazijahifadhiwa sehemu sahihi zikiwemo zilizokwisha muda wake.

KWIWEKO amesema kuwa kwa wafanyabiashara wanaojishughulisha na biashara ya vyakula, vipodozi na madawa wanapaswa kuwa na vibali kutoka TFDA.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive