AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA MAUAJI


Na Lilian Katabaro
KAHAMA.
 
Mkazi wa kijiji cha Bubungu Wilayani KAHAMA Mkoani Shinyanga, NAOMI MABULA (21) jana amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kahama kwa tuhuma za mauaji ya PASCHAL KASHINDYE.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo KENETH MUTEMBEI, mwendesha mashitaka wa Jeshi la Polisi MASAU MASATU amesema Machi 16 mwaka huu saa sita usiku katika kijiji cha Bubungu MABULA alimuua KASHINDYE kwa kutumia panga.

MASAU amesema NAOMI ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 196 sura ya 16 kanuni ya adhabu marejeo ya mwaka 2002.

Katika shauri hilo la jinai namba 07/2018, NAOMI hakutakiwa kujibu chochote kwasababu Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo ya mauaji.

NAOMI amerudishwa rumande na shauri hilo litatajwa tena Mahakamani hapo Machi 29 mwaka huu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive