HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA IKO MBIONI KUPOKEA TAKRIBANI MIL. 80 KWA AJILI YA KUKAMILISHA UJENZI WA ZAHANATI YA NYASUBI


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Halmashauri ya Mji wa KAHAMA Mkoani SHINYANGA inatarajia kupokea takribani shilingi milioni 80 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa zahanati ya NYASUBI ikiwa ni mikakati ya kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali ya halmashauri hiyo.

Akizungumza na KAHAMA FM, Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Dk. LUCAS DAVID amesema fedha hizo zinatolewa na serikali katika mwaka huu wa fedha 2017/2018.

Amesema itakapokamilika zahanati hiyo itasaidia kuwapunguzia wagonjwa wanaotoka eneo hilo, umbali mrefu wa kufuata huduma za afya sanjari na mpango wa kuboresha sekta ya afya katika kata mbalimbali za Halmashauri hiyo.

Wakizungumzia hatua hiyo, wakazi wa mjini Kahama, SOLOMON JUMA na SEBASTIANI MASHINJI, wameshauri Halmashauri hiyo kujenga zahanati na vituo vya afya katika kila kata ili kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali ya mji wa Kahama.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Kahama, ABEL SHIJA amewataka wananchi kuwa na subira kwani kwa sasa halmashauri hiyo inaendelea kuboresha ujenzi wa vituo vya afya katika kata zilizopo pembezoni mwa halmashauri hiyo.

Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kahama, inakadiriwa kuhudumia wagonjwa wasiopungua 1000 kwa siku hali inayosababisha msongamano mkubwa wa wagonjwa katika hospitalii hiyo.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive