AHUKUMIWA KWENDA JELA AU KULIPA FAINI KWA KOSA LA KUAJIRI RAIA WA KIGENI


Na Paulina Juma
KAHAMA.

Mkazi wa MALUNGA mjini Kahama HAMIDA JUMA amehukumiwa kwenda jela mwaka mmoja au kulipa faini ya Shilingi 500,000/= kwa kosa la kumuajiri raia wa BURUNDI asikuwa na kibali cha kuishi nchini.

Hukumu hiyo imetolewa jana na hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Kahama IMAN BATENZI baada ya HAMIDA kukiri kutenda kosa hilo mahakamani hapo.

Awali mwendesha mashitaka wa idara ya Uhamiaji SALUM RASHID amesema HAMIDA alikamatwa April 6 mwaka huu saa 4 asubuhi huko Malunga akiwa amemuajiri kufanya kazi za mamalishe raia huyo wa Burundi.

SALUM amesema HAMIDA amefanya kosa hilo kinyume na kifungu cha 45 na kifungu kidogo cha 2 cha sheria ya uhamiaji namba 7 ya 1995 iliyofanyiwa marekebisho 2016.

Katika shauri hilo la jinai namba 47/2018, HAMIDA ameshindwa kulipa faini na ameanza jana kutumikia kifungo hicho jela.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive