AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA KWA KOSA LA KUMUUA MTOTO



Na Lily/Danny
KAHAMA

Mkazi wa kata ya Nyasubi mjini Kahama Mkoani Shinyanga, SAMSONI BWIRE (60) amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mtoto DEVOTA GERARD(4) kwa makusudi.

Hukumu hiyo imetolewa na Jaji wa Mahakama kuu kanda ya SHINYANGA, RICHARD KIBELLA baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi tisa wa upande wa jamhuri ambao wamethibitisha kosa hilo pasipo kuacha shaka yeyote.

KIBELLA amesema mashahidi hao wameithibitishia Mahakama hiyo kuwa BWIRE alimuua kwa makusudi DEVOTA GERARD kwa kutumia panga May 16/2013 katika kata ya Nyasubi Mjini Kahama huku akijua kuwa ni kosa kisheria.

Jaji KIBELA amesema mahakama hiyo imetoa adhabu hiyo ili iwefundisho kwake na kwa watu wengine kwenye jamii ambao wanajichukulia sheria mkononi na kuwadhuru watu wengine kwa maslahi yao binafsi.

Awali akisoma maelezo ya shauri hilo la mauaji namba 23/2013 wakili wa Selikali, UPENDO SHEMKOLE amesema BWIRE amekiuka kifungu cha sheria namba 196 na 197 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002 na kuiomba kutoa adhabu kali.

Nae wakili wa utetezi FESTO LEMA ameiomba mahakama kumpunguzia adhabu mteja wake kwani anafamilia inayomtegemea na ni kosa lake la kwanza hoja ambayo imetupiliwa mbali na Mahakama hiyo.

BWIRE ameanza jana kutumikia adhabu hiyo.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive