AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA KUZINI



Na Daniel Magwina
KAHAMA.

Mkazi wa kijiji cha Sangilwa Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA, JUMANNE KUSINZA (35) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya kuzini maharamu kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo IMANI BATENZI, mwendesha mashitaka SAADA ADAM amesema KUSINZA kwa nyakati tofauti mwezi Agost na Septemba mwaka jana huko Sangilwa, alimbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 8 mwanafunzi wa darasa la kwanza.

SAADA amefafanua kuwa KUSINZA ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 158 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

Katika shauri hilo la jinai namba 131/2018, KUSINZA amekana kutenda kosa hilo na upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na mshitakiwa amerudishwa rumande kwa kukosa dhamana hadi Aprili 5 mwaka huu shauri hilo litakapotajwa tena.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive