AHUKUMIWA KWENDA JELA AU KULIPA FAINI KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI KINYUME NA SHERIA



Na Paulina Juma
KAHAMA.

Raia wa Burundi, EDSON AJUAE (19) jana amehukumiwa kwenda jela mwaka 1 au kulipa faini ya shilingi 500,000 kwa kosa la kuwepo nchini kinyume na sheria ya Uhamiaji.

Akitoa hukumu hiyo leo, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya wilaya ya Kahama, IMANI BATENZI amesema ametoa hukumu hiyo baada ya AJUAE kukiri kutenda kosa hilo mahakamani hapo.

Awali, Mwendesha Mashitaka wa Idara ya Uhamiaji, SALUMU RASHID amesema AJUAE alikamatwa March 13 mwaka huu majira ya saa 3 asubuhi maeneo ya Line Police mjini Kahama akiwa hana kibali chochote cha kuwepo nchini.

Katika shauri hilo la jinai namba 110/2018, AJUAE ametenda kosa kinyume na kifungu namba 45 cha sheria ya Uhamiaji namba 7 ya mwaka 1995 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016.

AJUAE ameshindwa kulipa faini na ameanza kutumikia kifungo hicho leo na mara baada ya kumaliza kifungo hicho atarejeshwa nchini kwao BURUNDI.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive