WANANCHI WALIOVAMIA ENEO LA MGODI WA ACACIA BULYANKULU WAAMRIWA KUONDOKA


Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Zaidi ya wachimbaji wadogo wa madini 800 waliovamia eneo linalomilikiwa na mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyankulu katika Halmashauri ya Msalala, Wilayani Kahama wameamriwa kuondoka katika eneo hilo mara moja.

Agizo hilo limetolewa leo na Mkuu wa wilaya ya Kahama FADHILI NKURLU wakati akizungumza na waandishi wa Habari kuhusiana na namna zoezi hilo litakavyotekelezwa.

Amesema ingawa ramani inaonesha kuwa eneo hilo liko ndani ya leseni ya Acacia mkazi mmoja alijenga nyumba katika eneo hilo kwa lengo la kuishi na badala yake alianza kuchimba dhahabu hali iliyosababisha wachimbaji wengine kulivamia.

Wavamizi hao wamefanya uharibifu mkubwa wa ardhi kwa kuchimba mashimo mengi ambayo kwa mujibu wa NKURLU ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kahama yatafukiwa kesho ili kuzuia madhara kwa binadamu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels