WANANCHI WA HALMASHAURI YA MSALALA WILAYANI KAHAMA WATAKIWA KUJIANDAA NA ZOEZI LA UANDIKISHAJI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA

Image result for VITAMBULISHO VYA TAIFA
Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Serikali Wilayani KAHAMA imewataka wananchi wa Halmashauri ya Msalala Wilayani wilayani humo kujiandaa na zoezi la uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa linalotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa wilaya hiyo, FADHILI NKURLU wakati akizungumza na waandishi wa Habari mjini Kahama kuhusiana na namna zoezi hilo litavyotekelezwa na kusema kuwa Halmashauri ya mji wa Kahama inaelekea kuhitimisha zoezi hilo hivi karibuni.

Amesema zoezi hilo linatekelezwa na Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) na linafanyika bure na hakuna mwananchi atakayetozwa gharama yeyote hivyo wanapaswa kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo.

Amefafanua kuwa Mpaka sasa Halmashauri ya Mji wa Kahama imeandikisha watu elfu 99 na 750 sawa na asilimia 87 ya lengo liliowekwa la kuandikisha watu laki 1 na 14 elfu 260.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels