AHUKUMIWA KWENDA JELA MIEZI SITA AU KULIPA FAINI KWA KOSA LA KUWEPO NCHINI KINYUME CHA SHERIA



Na Paulina Juma
KAHAMA.
 
Raia wa Burundi, NSABIMANA RAMADHAN (23) amehukumiwa kwenda jela miezi 6 au kulipa faini ya shilingi 500,000 kwa kosa la kuwepo nchini kinyume na sheria ya uhamiaji.

Huku hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA IMANI BATENZI, baada ya NSABIMANA kukiri kutenda kosa hilo.

Awali mwendesha mashitaka wa Idara ya Uhamiaji, SALUMU RASHID amesema RAMADHAN alikamatwa April 10 mwaka huu maeneo ya Soko kuu mjini Kahama akiwa hana kibali kinachomruhusu kuwepo nchini.

Katika shauri hilo la jinai namba 149/2018, RAMADHAN ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 45 cha sheria ya uhamiaji namba 7 ya mwaka 1995 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016.

RAMADHAN ameshindwa kulipa faini na ameanza kutumikia kifungo cha miezi 6 jela na mara baada ya kumaliza kifungo hicho atarejeshwa nchini kwao Burundi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels