Naibu Waziri Shonza Awataka Wasanii Kujijengea Tabia Ya Kujiwekea Akiba

Naibu waziri wa Habarui, sanaa utamaduni na michezo Mhe. Juliana Shonza amewataka wasanii wa Injili kjijengea tabia ya kujiwekea akiba ili punde wapatapo matatizo waweze kuyatatua kwa urahisi.

Ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizindua mfuko wa Tagoane LoanFund Jijini Arusha ambapo amepongeza uongozi wa Tagoane kufikia hatua hiyo. Ameyataka mashirikisho yote ya muziki wa Injili nchini Tanzania kuiga mfano nzuri wa Tagoane ili waweze kuwa na mashirikisho ambayo ni hai na yanayoleta mshindo kwenye jamii.

Amesema yeye kama mlezi wa wasanii wote nchi amewaomba waamke wachangamkie fursa na wasiwe wavivu kujifunza kutoka kwa wenzao waliofanikiwa .Amewataka wasanii kukaa kwa pamoja Kuonyeshe Uzalendo kwa nchi yao wajadili changamoto mbalimbali wanazozipitia na kutafuta namna ya kutazua changamoto zinazowakabili.

Kwa upande wake Rais wa Tagoane Taifa Dkt. Godwin Maimu amesema kuwa wanedhamiria kuanzisha mfuko wao wa Tagoane Loan Fund ambapo mpaka sasa umekuwa na wanachama ambao wameshachangia akiba zao zipatazo shilingi milioni kumi.Amesema mfuko huo unatarajiwa kuanza kutoa mikopo kwa wanachama wavhqngiaji kuanzia 2 januari 2019

Maendeleo kama vijana hayawezi kuendelea ukiwa na jitihada za mtu mmoja mmoja bali balintunapounganisha nguvu zetu kwa pamoja mwisho wa siku tunapata kitu cha kuweza kutusaidia. Alisema Dkt Maimu

Amesema lengo la mfuko huo ni kuwakwamua wasanii watakaokuwa na miradi ya uwekezaji, makampuni makubwa, na watakaoweza kutoa fursa na ajira kwa vijana hapa nchini na kulipa kodi kama wananchi wengine

Aidha tamasha hilo lililoshorikisha wasanii mbalimbali wakiwemo wajasiriamali, wachoraji, wachongaji, sanaa za ubunifu ni fursa ambayo Tagoane wameileta na kuwataka wasanii waitumie kwaajili ya kujikwamua kiuchumi na kuoata maendeleo katia jamii nzima

Tamasha hilo la Tukuza festival lilizinduliwa rasmi mwaka 2017 likiwa linafanyika kwa mara ya pili limebeba kauli mbiu isemayo toto yatima haihitaji chakula a mavazi peke yake ila awezeshwe nyenzo za kutimiza malengo yake.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels