Rais Magufuli Akerwa na Viongozi Anaowateua Kuanza Kugombana Badala ya Kufanya Kazi

Rais John Magufuli ameweka wazi kwamba hafurahishwi na migogoro kati ya viongozi anaowateua na kusema kuwa amewaweka kiporo Mkuu wa Wilaya  na Mkurugenzi wake kutokana na matendo yao ya kugombana badala ya kufanya kazi hivyo wasifikiri kwamba hafahamu.
 
Rais Magufuli ameyasema hayo jana baada ya kumaliza kuapisha viongozi wapya aliowateua baada ya kufanya mabadiliko katika Wizara mbalimbali pamoja na Makatibu wa Wizara.

Rais alisema kwamba anafahamu changamoto ni nyingi katika utendaji wa kazi ingawa yapo mengine mazuri wanayofanya na kuwataka wahakikishe wanajitoa kwa maslahi ya wananchi.

"Nafahamu hizi kazi zina changamoto nyingi sana mfano kuna DC Gairo na Mbunge hawaelewani mpaka Mbunge anapost kumtukana DC tena mke wa mtu, hajui kama anaweza upoteza Ubunge, "I hope' siku moja ataomba msamaha kwenye Bunge", alisema Mh Rais Magufuli na kuongeza;

"Halmashauri ya Nyasa wanagombana sana DC na Mkurugenzi, nimewaangalia tu! nimewaachia kiporo chao. Pale Dodoma Mkurugenzi wa Jiji na DC walikuwa wanagombana nika-send meseji nikawaambia endeleeni kugombana siku moja mtagombania Vijijini, wamenyamaza naona yameisha".
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels