Lugola Awataka Polisi Watafute Njia Mbadala ya Kuwakamata Bodaboda Badala ya Kuwavizia na Kusababisha Ajali


Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amewataka polisi kuja na njia mbadala za kuwakamata madereva bodaboda badala ya kuwavizia kwenye minada na magulio na kusababisha ajali.

Lugola amesema hayo jana Jumatano Januari 2, 2019 Bukoba mkoani Kagera katika mkutano wa hadhara.

Amesema hakuna ulazima wa kufukuzana na waendesha pikipiki kwa kuwa vyombo wanavyoendesha vinaweza kuchukuliwa namba kuliko kuwavizia na kufukuzana nao.

Ameonya hatua ya kuwavizia kwenye minada, magulio na maeneo mengine inawaathiri hata abiria wanaokuwa wamebebwa katika pikipiki hizo kwa kupata ajali.

Katika mkutano huo wa hadhara uliofanyika uwanja wa Mashujaa baadhi ya waendesha pikipiki wamedai hakuna mazingira rafiki ya kufanya kazi kati yao na Polisi.

Hata hivyo, Waziri Lugola amewataka waendesha pikipiki kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kulinda haki za watumiaji wengine wa barabara.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels