DIWANI KAHAMA AANGUA KILIO KWENYE BARAZA LA MADIWANI,AKILALAMIKIA HOJA YAKE KUTOPEWA NAFASI


DIWANI WA KATA YA SABASABINI HALMASHAURI YA USHETU EMMANUEL MAKASHI ALIYEANGUA KILIO KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

Na Salvatory Ntandu
KAHAMA
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Diwani wa Kata ya Sabasabini EMANUEL MAKASHI amengua kilio  kwenye kikao cha Baraza la Madiwani alilalamikia hoja yake kutopewa nafasi ya kusikilizwa katika kikao hicho  aliyoiwasilisha juu ya kutoridhishwa na utendaji kazi  wa afisa Mtendaji wa Kata hiyo CHRISTOPER LYOGELO.
Katika Madai aliyoyawasilisha MAKASHI amesema tangu afisa huyo apangiwe katika kituo hicho cha kazi mwaka 2005 ,amekuwa hasomi mapatao na matumizi, hali ambayo imesababisha wananchi kugoma kuchangia shughuli za maendeleo.
Baada ya kumsikiliza MAKASHI hatimaye hoja hiyo imejibiwa na Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu ONESMO BENJAMIN  na haya hapa majibu yake aliyoyatoa kwenye kikao.
Amesema watahakikisha suala hilo linafanyiwa kazi kwa haraka ili muafaka upatikane.
Lakini baaada ya kumalizika kwa kikao hicho cha Baraza la Madiwani Raha ya leo ilimtafuta MH.MAKASHI kuzungumzia hoja aliyoiwasilisha katika Baraza hilo.
Baraza la Ushetu limeketi kwa siku mbili kwa wakilishi wananchi(madiwani) kujadili taarifa mbalimbali kuhusiana na maendeleo ya wananchi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels