WAZEE KAHAMA WATAJWA KUWA NA NAFASI YA KUIMARISHA MILA NA DESTURI

Wazee  wilayani Kahama mkoani Shinyanga, wametajwa kuwa na nafasi kubwa ya kuimarisha mila na desturi katika jamii endapo waataendelea kusimamia  na kuelekeza maadili mema kwa jamii.
Hayo yameelezwa hivi karibuni na  Katibu wa Umoja wa  wazee wilaya ya Kahama (UWAKA) PAUL NTELYA wakati akizungumza kwenye  Uzinduzi wa tawi la umoja huo kata ya Bulungwa halmashauri ya Ushetu.
NTELYA amesema ili kuwa na taifa lenye watu waadilifu ni lazima wazee wachukue nafasi ya kukemea maovu yote yanayoharibu maadili mema katika jamii na kwamba jamii izidi kudumisha mila na desturi zao.
 
Katika huzinduzi huo wa tawi  la UWAKA kata ya Bulungwa, umeundwa uongozi wa  Kata hiyo ambao utaratibu shughuli zote zinazuhusu umoja huo ikiwamo kutetea haki za  wazee hasa katika upande wa matibabu na migogoro ya ardhi.
Mwneyekiti wa UWAKA , Kata ya Bulungwa,  KAGEMO KAYANDA, amewaomba  wazee katika kata hiyo kuwa na umoja ili kuisdaidia jamii katika masuala mbalimbali ikiwamo suala la Migogoro ya Ardhi ambalo limekuwa ni tatizo kubwa katika maeneo mengi nchini.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels