BODI YA ELIMU MSALALA KAHAMA YAKABIDHI MADAWATI 160 KATIKA SHULE TATU ZA SEKONDARI

Zaidi ya madawati 160 yamekabidhiwa na bodi ya elimu-Msalala, katika shule tatu za Secondari za halmashauri ya hiyo ili kupunguza tatizo uhaba wa madawati kwa shule za sekondari.
Akizungumza leo katika makabidhiano ya madawati hayo kaimu katibu wa bodi ya elimu Msalala MASATU MNYORO  amezitaja shule zilizokabidhiwa madawati hayo  kuwa ni  shule ya sekondari Segese, Isaka na   Mwalimu nyerere.  
MNYORO amesema  halmashauri hiyo, imekusudia kuboresha sheria  ya  mfuko wa elimu ili iwe na vyanzo vingi vya mapato na kwamba amewataka walimu wakuu  kusimamia utunzaji wa madawati hayo.
Kwa upande wao walimu wakuu wa shule hizo wameishukuru Halmashuri hiyo na kwamba madawati hayo yatasaidia kupunguza changamato ya madawati.
Naye mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya msalala SIMON BEREGE amewataka wadau mbali mbali kushirikiana kwa pamoja ili kujenga vyumba vya madarasa na madawati ili kuondokana na tatizo hilo.
Bodi ya mfuko wa elimu kwa Halmshauri ya msalala ilianza kufanya kazi mwaka 2016 kwa kuhakikisha inaboresha miundombinu ya elimu na kutafuta fedha kwa ajili ya kutengeneza madawati, kujenga maabara na vyumba vya madarasa.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels