WAANDISHI WA HABARI WANAWAKE WATAKIWA KUTUMIA TAALUMA ZAO KUPATA VYEO NA SIYO KUFANYA MAPENZI NA WAAJIRI

BI ROSE HAJI MWALIMU  AKIWASILISHA MADA KWENYE MAFUNZO YA TATHIMINI NA UFUATILIAJI KWA WANDISHI WA HABARI MJINI DODOMA 



Wandishi wa habari wanawake nchini  wametakiwa kutumia uwezo wao kitaaluma wanapotekeleza majukumu yao wawapo kazini na si kujiingiza katika masuala ya mapenzi na waajiri wao ili wapandishwe vyeo.

Hayo yamesemwa na  mkufunzi wa Radio za kijamii nchini Kutoka Unesco Bi Rose Mwalimu kupitia semina ya radio za kijamiii iliyofanyika ukumbi wa wakala wa majengo  mjini Dodoma ambayo ilikutanisha vituo 24 vya radio za kijamii .

 

Akiwasilisha mada ya maadili kupitia semina hiyo Bi Rose amesema  wazazi na walezi wamewasomesha watoto wao ili waweze kupata taaluma na kurudi katika jamiii  kuitumikia  ikiwa ni paamoja na kujipatia kipato badala yake wandishi wengi wanawake wamekuwa wakishindwa kutumia elimu waliyoipata katika utendaji kazi 


Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa semina hiyo wamesema kuwa wanawake wengi hushindwa kufanya kazi zao vizuri kutokana na tamaa  za maisha kwa sababu huhitaji kupata  pesa amabazo ziko nje ya uwezo wao.

 

Mafunzo hayo yameanza  Februari 6, 2018 na yanatarajiwa kumalizika tarehe 12 Februari 12, siku moja kabla ya maadhimisho ya siku ya radio duniani.


MATUKIO KATIKA PICHA:


WANDISHI WA HABARI WA REDIO ZA KIJAMII WAKIWA KWENYE MAFUNZO YANAYOENDELEA MJINI DODOMA 

WANDISHI WA HABARI ZA REDIO ZA JAMII KUTOKA MAENEO TOFAUTI YA TANZANIA WAKIWA KWENYE MAFUNZO YANAYOENDELEA  MJINI DODOMA


MWALIMU MARKO AKIWA ANATAYARISHA MADA KWA AJILI YA KUIWASILISHA KWA WANDISHI WA HABARI WA REDIO ZA JAMII TANZANIA KWENYE MAFUNZO YANAYOENDELEA MJINI DODOMA

Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels