KUWASA YAPATA HASARA YA SHILINGI MILIONI 106 BAADA YA KUKOSEKANA KWA MAJI MJINI KAHAMA KWA SIKU 12

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mjini Kahama, (KUWASA) imepata hasara ya  takriban shilingi milioni 106 kutokana na ukosefu wa maji ulioukumba mji wa Kahama kwa takriban siku 12.

Hayo yamebainishwa na  Kaimu Mkurugenzi wa KUWASA, Mhandisi  CHANGANYA PAUL katika mkutano wake na Wandishi wa Habari kuzungumzia athari zilizotokana na kusitishwa kwa huduma hiyo na jinsi Mamlaka ilivyojipanga kukabiliana na hali hiyo siku za usoni.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa  Bodi ya Wakurugenzi ya KUWASA, Meja Mtaafu BAHATI MATALA amesema wanafanya mazungumzo na KASHWASA ili  kutafuta nishati  mbadala ya umeme kwenye chanzo kikuu cha maji ya ziwa Viktoria kilichopo Ihelele wilayani Misungwi mkoani Mwanza.


Januari 17 mwaka huu, Shirika la Umeme TANESCO lilisitisha huduma ya umeme kwenye chanzo hicho cha Ihele,  kutokana na  deni la zaidi ya shilingi bilioni mbili wanaloidai KASHWASA  hatua iliyosababisha mji wa Kahama kukosa maji kwa takriban siku kumi na mbili na hivyo uzalishaji wa maji kusimama kabisa.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels