AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA WIZI


Na Lilian Katabaro
KAHAMA.

Mkazi wa mtaa wa Mhongolo katika Halmashauri ya Mji wa KAHAMA Mkoani SHINYANGA ALLY SINGA (26) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya wizi wa kuaminika kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo KENETH MUTEMBEI, mwendesha mashitaka wa Jeshi la Poilisi PETER MASAU amesema Mei 4 mwaka huu saa sita mchana maeneo ya uzunguni mjini Kahama, ALLY aliiba pikipiki aina ya SUN LG - MC 450 BRS.

MASAU amesema pikipiki hiyo yenye thamani ya shilingi milioni mbili ni mali ya JUMA MARCO aliyekuwa amemuamini ALLY na kumpa aendeshe kama bodaboda na badala yake akaitumia kwa matumizi yake binafsi.

Katika shauri hilo la jinai namba 188/2018 ALLY ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 273 sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

ALLY amekana kutenda kosa hilo na upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na mshitakiwa amerudishwa rumande kwa kukosa dhamana na shauri hilo litatajwa tena Mei 31 mwaka huu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive