MADEREVA BAJAJI WAILALAMIKIA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA KWA KUSHINDWA KUREKEBISHA BAADHI YA BARABARA AMBAZO NI MBOVU


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Baadhi ya madereva wa magari na waendesha pikipiki za magurudumu matatu, (BAJAJI) Mjini KAHAMA wameilalamikia Halmashauri ya Mji wa KAHAMA kwa kushindwa kuyakarabati makaravati mbalimbali yaliyopo katika barabara licha ya kuwa yamevunjika muda mrefu.

Madereva hao, YUSUPH SAID, JOHN ROBERT na RAMADHAN NKANDI, wamesema wamekuwa wakipata usumbufu wakati wa kutumia barabara ambazo makaravati yake yamevunjika ikiwamo barabara ya kutoka lilipokwa soko la wakulima kwenda Standi ndogo ya mabasi iliyopo Majengo mjini humo.

Naye Katibu wa madereva wa magari madogo ya abiria yanayosafirisha abiria kati ya Kahama na Shinyanga, JUMANNE SONGORO amesema kutokana na ubovu wa makaravati mawili yaliyopo katika barabara ya kutoka Isaka kwenda Standi ndogo ya majengo ajali mbalimbali zimekuwa zikitokea.

Meneja wa wakala wa barabara za mjini na vijijni TARURA halmashauri ya Mji wa Kahama, Mhandisi JOB MUTAGWABA amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo ambapo amesema katika bajeti ya mwaka 2017/2018 zaidi ya shilingi milioni 60 zimetengwa kuboresha makaravati yote ya mjini Kahama.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive